Tiba asilia ya matatizo ya macho


Karoti, maji, "majani", dawa kiboko ya macho???

Kwa wanaopenda tiba natural (asili) kwa macho yanayouma na kutoa machozi tumieni karoti kila siku (japo mzizi mmoja), kunywa maji ya kutosha na mboga za majani (zisiive sana).

Macho yako yatarudia uimara madhubuti na hutahitaji kumeza vidonge tena. Tiba hii nimetumia mimi mwenyewe na imenifaa sana. Jaribu tiba asili ya chakula kabla ya kukimbilia dawa kali.



Je unasumbuliwa na macho?Rejesha uwezo wako .???

Tatizo la kutokuona vitu vizuri halitokani na misuli ya macho kulegea, bali uchovu, hivyo unatakiwa u-relax .

Wakati uko kwenye msongo wa mawazo misuli inayozunguka mboni ya jicho hubanwa na kuikosesha utulivu, hii husababisha kupungua kwa uwezo wa jicho kuona/kuona vitu kama vina ukungu(blur vision) na kuwa unabadilika mahali ambapo uoni unakuwepo kwenye retina.

Matatizo ya kuona masafa ya karibu, mbali, mbali na karibu(astigmatism), mtoto wa jicho(catalact) na glaucoma yanaweza kutokomezwa kwa "Dr. Bates method).
Nyoosha kiganja chako vidole vikiwa vimefunga kisha tumia vitundu vidogo katikati ya vidole kutazama vitu utaona kwamba uwezo wako wa kuona unaweza kurejea kama awali.

"Dr. Bates method" ni mbinu ya kiakili inayokufundisha namna ya kuondoa uchovu kwenye misuli ya macho yako na kurejesha uoni wako uliopungua.


NI KWA NAMNA GANI BATES METHOD INAFANYA KAZI?

"Kwa kawaida jicho lako limezungukwa na misuli sita na inatembea kuzunguka jicho lako. Kwa kawaida mishipa hiyo huwa rahisi kufuata kile jicho lako linata kukiona.

Tatizo linaweza kutokana na sababu za hisia za kimwili(hofu, msongo wa mawazo, hasira nk)" .
Anasema Dr. Bates.
Kwahiyo una machaguo matatu...

1. Kufahamu tatizo linalokufanya uwe msongo wa mawazo. Unapoondokana na msongo wa mawazo na kuifanya akili itulie/relax mara uwezo wa kuona vizuri hurejea kama mwanzo.

2. Kufanya upasuaji(LASIK) ambao hubadili moja kwa moja uwezo wa macho ku-focus mbali.


3. Kuvaa miwani(contact lens). Kuvaa miwani hufanya tatizo liwe endelevu kwa sababu miwani haiondoi tatizo zaidi ya kukufanya uwe tegemezi.

Wakati watu wanaposhindwa kuona vitu vizuri hujikuta wakibinya macho ili kufanya vitu kuonekana vizuri. Kubinya macho ni tendo baya ambalo hufanya mhusika kuwa stressed na hivyo kubana misuli kuzunguka mboni ya jicho.


Moja ya mbinu iliyotumiwa na Dr. Bates kwa wagonjwa wake ni njia ya viganja(Palming). Tazama mahali kisha angalia uwezo wako wa kuona mwanzoni ulivyo. Taratibu weka viganja vyako juu ya macho yako kisha tulia(relax), regeza mabega yako.

 Unaweza kujiegemeza kwenye meza au juu ya mto ili kuongeza utulivu(relaxion). Tulia(relax) walau kwa muda wa dakika mbili kisha ondoa mikono yako juu ya macho kisha angalia kama kuna vitu vinaonekana vizuri tofauti na kabla huja-relax.

Chukua karatasi yenye maandishi kisha isogeze karibu kabisa na pua(kwa wenye mypoia& astigmatism)utakuwa unayaona maandishi vizuri kisha haraka sana isogeze mbali karatasi hiyo bila kupepesa macho pembeni, endelea kutazama hadi pale utakapoona mabadiliko kidogo kisha utoe karatasi. Kwa wenye presbyopia(kutokuona vitu vya karibu) chukua karatasi yenye maandishi yanayosomeka vizuri kisha iweke mbali mbele ya macho kwa muda kisha ghafla ihamishe karibu na uso. Fanya hivyo mara kwa mara hadi tatizo litakapoisha.


Dr. Bates anasema kwamba jicho haliwezi ku-focus kwenye vitu vinavyonekana bali, hutaka kuona vitu visivyoonekana hivyo unapotazama karatasi yenye maandishi au kitu chochote kwenye umbali usioweza kuona vizuri hufanya mishipa ya fahamu iliyounganika na jicho hupeleka taarifa kwenye ubongo na ubongo hurudisha jibu kwamba umeona kitu hicho hivyo baada ya muda vitu hivyo vitaanza kuzoeleka kwenye ubongo (rejea kwamba matatizo ya uwezo wa kuona hutokana na uchovu kwenye mishipa inayozunguka macho kuzuia kupeleka taarifa ya taswira kwenye ubongo), kwahiyo hata pale unapotumia miwani kurekebisha uoni wako, taarifa hupelekwa kwenye ubongo kwamba taswira imeonekana kwa msaada wa miwani na hivyo kufanya uendelee kuwa tegemezi kwa miwani huku tatizo likiendelea kuwepo.


NOTE

Njia ya Dr. Bates sio mbinu kitabibu bali ni mbinu ya kiakili, kwahiyo hakikisha unatambua tatizo lako kwa kuonana na daktari macho kupata vipimo. Zoezi hili linahitaji uvumilivu na baada ya muda matokeo yatakuwa mazuri.
Unaweza kuangalia video hizi namna ya kufanya mazoezi hatua kwa hatua hadi kupona kabisa tatizo lako.

Watakaoanza kutumia njia hii ya Dr. Bates ni vizuri wakawa wanaleta mrejesho hapa ili wengine wahamasike kutumia njia


Kuwa na macho mekundu na tiba yake????

TIBA ( 1)

 Weka macho yawe safi n uyakoshe kwa maji ya waridi kila wakati. Epusha macho kutokana na joto, baridi, moshi, vumbi, macho yasitumie nguvu sana kama vile kusoma sana. Tumia dawa za kulainisha choo ikiwa hupati choo vizuri kwa sababu pia huchangia katika maumivu ya kichwa na macho.aw pia anakula karoti.:


Tiba (2)

 Matatizo ya macho Asali ni bingwa kwa ajili ya macho, Pakaa asali katika macho huzidisha nuru ya macho, pia husaidia katika matibabu ya trachom conjuctivits na maradhi mengine ya macho, kila siku pakaa asali katika nje ya jicho na ndani ya jicho (kwa ndani ya jich unaweza kutumia unyoya au wa kuku au ndege yoyote yule) kufanya hivo asali hupigana na kujilinda na maradhi ya glaucoma.


Tiba (3)

 Asali pia husaidia kwa matatizo ya cataract, chukua 2 grams ya maji ya vitunguumaji na asali uchange pamoja upake hii kwa wale wenywe immature cataract.

 (Upate Asali ya nyuki mbichi tena iwe Safi ) isiyochanganywa na sukar Chaguwa moja kati ya hizo Tiba hapo juu tumia kwa muda wa siku 3 isipomfaa ndio unatumia Tiba ingine.


Tiba asilia ya matatizo ya macho Tiba asilia ya matatizo ya macho Reviewed by Cadotz media on February 05, 2019 Rating: 5

No comments

Ndugu ahsante kwa kuitembelea Cadotz, Endelea kufurahia huduma zetu pia Tunakusogezea Cadotz uchague unachokitaka katika menyu zetu.
Bofya chini

MIZIKI | MAPENZI | AFYA